Ndio, unatakiwa kuendelea na unyonyeshaji huku ukizingatia mwongozo wa kujikinga na Corona. Utafiti uliofanyika mpaka sasa haujagundua uwepo wa maambukizi ya COVID-19 kupitia maziwa ya mama na unyonyeshaji.
Uvaaji wa barakoa, kunawa mikono na sabuni na maji tiririka kabla na baada ya kumshika mtoto , usafi wa mara kwa mara wa mazingira kuua vijinunu unaendelea kumiziwa. Kifua cha mama kinatakiwa kusafishwa iwapo tuu amekoholea eneo hilo, ziwa la mama halihitajiki kusafishwa kila anapotaka kunyonyesha mtoto.
Ninaweza kupata chanjo ya Corona wakati nanyonyesha?
Ndio, wataalamu wa afya wanahimiza wakina mama wanao nyonyesha au kukamua maziwa kupata chanjo ya COVID-19